Saturday, June 30, 2012

NO VIZA NO BET KWA CAMP MULLA


Camp Mulla music group inayofanya poa sana kutoka Kenya ambao wamechaguliwa kugombea tuzo za BET mwaka huu, hawatafanikiwa kuhudhuria tuzo hizo badala yake watajua matokeo yao wakiwa mbele ya TV zao hapo hapo Kenya 
kuna habari kuwa group hilo limeshindwa kufanya process ya visa mapema, matokeo yake wakaamua kuomba special case visa wakiwa na kichwa cha habari walichoandika "major awards show nomination" kama sababu.
special case visa huwa zinatolewa kwa wanaosafiri kwasababu za kimatibabu, hifadhi za kisiasa, apointment za utawala wa kisiasa mfano diplomats. camp mulla walijaribu kwenda mapema ubalozini kabla ya siku ya interview lakiini waliambiwa hawawezi kufanyiwa interview tofauti na siku waliyopangiwa
Pamoja na hayo camp mulla wanaweza wakapata viza lakini itakua ni baada ya show ya tuzo hizo kufanyika na washindi kutangazwa. Group hilo linaundwa na Taio Tripper, Shappaman Kass, K'Cous and Miss Karun wakiwa ni group la kwanza kutoka EA kuchaguliwa katika tuzo hizo.
na dj Fetty

No comments:

Post a Comment