MJENGO ambao wataishi washiriki wa Epiq Bongo Star
Search 2012, umeleta mzuka kwa baadhi ya washiriki ambao wameazimia
kujifua kuhakikisha wanatimba kula bata.Wakipiga
stori na Showbiz kwa nyakati tofauti, baadhi ya washiriki hao kutoka
mikoa mbalimbali walisema jumba hilo limewapa ari na nguvu mpya kufanya
mazoezi ya kutosha kuhahakisha wanaingia na kudumu ndani ya mjengo huo
kabla ya kung’ara kitaani.Jengo hilo lilianikwa hivi karibuni licha ya kwamba haikufahamika liko maeneo gani na kwa nje linaonekana ni la kifahari kiasi cha baadhi ya watu kudai kuwa, mandhari ya ndani yanaweza kuwa kama ya lile la Big Brother.
No comments:
Post a Comment