Sunday, April 29, 2012

CONFIRMED

Zijue baadhi ya sababu na madhra ya utumiaji wa madawa ya kulevya

Ukosefu wa ajira

Nchini Tanzania kiwango cha ukosefu wa ajira kimo juu sana.Ukosefu wa ajira umesababisha vijana wengi kukaa ovyo bila chochote cha kufanya na kugeukia madawa ya kulevya.

Shinikizo kutokana na marafiki.

Hii ni moja ya sababu kuu ya kutumia madawa ya kulevya. Wengi wanaotumia madawa ya kulevya katika ukanda huu wamekubali kwamba walianza kutumia madawa kwa sababu wengi marafiki wao walikuwa wanatumia .Wengi wa vijana ambao wanapatikana maeneo ya baharini wanatumia madawa haya ili wapate ujasiri wa kuzungumza na wateja wao.

Athari:

 Uhalifu

Nchini Tanzania, vijana wengi hawawezi kukaa bila kutumia dawa hizi. Dawa hizi huwa ghali mno na la kusikitisha ni kuwa vijana hawa hawana ajira. Hiii inamaanisha kuwa vile wanavyoweza kupata pesa ni kwa kuwaibia wakazi wenzao. Hii inasababisha hali ya usalama nchini kutoaminika.

Maradhi

Hii ni athari kubwa ya madawa ya kulevya. Kuna maradhi mengi ambayo vijana hawa wanapata kutokana na madawa haya. Baadhi yao wamekuwa wendawazimu. Maradhi haya yanawapata vijana kwa kasi mno kwa sababu ya kutokula vyema.Hawa vijana hawali lakini wanaendelea kutumia madawa haya.Pia wanaambukizana maradhi kwa kubadilishana sindano. Hii imesababisha kuzidi kusambaa kwa UKIMWI nchini.

Kifo

Mwishowe athari hizi zote zaelekeza kaburini. Kiwango cha vifo Tanzania kinaongezeka kwa kasi mno. Vijana wengi nchini  wanaaga dunia katika miaka yao ya thelathini.Vifo hivi vinasababishwa hasa na maradhi yanayoletwa na madawa ya kulevya. Hili ni jambo linatia nchi ya Tanzania wasiwasi kwani vijana wengi ambao ni nguvukazi ya taifa wanaaga dunia.

No comments:

Post a Comment